Yohana
12:32 - Nami nikiinuliwa juu ya nchi,
nitawavuta wote kwangu.
1
Wakorintho 1:17 - Maana
Kristo hakunituma ili nibatize, bali niihubiri Habari Njema; wala si kwa
hekima ya maneno, msalaba wa Kristo usije ukabatilika.
1
Wakorintho 1:27-29 - Bali
Mungu aliyachagua mambo mapumbavu ya dunia awaaibishe wenye hekima; tena
Mungu alivichagua vitu dhaifu vya dunia ili aviaibishe vyenye nguvu; tena
Mungu alivichagua vitu vinyonge vya dunia na vilivyodharauliwa, naam, vitu
ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko; mwenye mwili awaye yote
asije akajisifu mbele za Mungu.
1
Wakorintho 2:4 -Na neno langu na kuhubiri kwangu
hakukuwa kwa maneno ya hekima yenye kushawishi akili za watu, bali kwa
dalili za Roho na za nguvu,
Ayubu
11:18, 19 - Nawe utakuwa salama, kwa sababu
kuna matumaini; Naam, utatafuta-tafuta kando yako, na kupumzika katika
salama. Tena utalala, wala hapana atakayekutia hofu; Naam, wengi
watakutafuta uso wako.
Zaburi
3:5 - Nalijilaza nikalala usingizi,
nikaamka, Kwa kuwa Bwana ananitegemeza.
Zaburi
4:8 - Katika amani nitajilaza na
kupata usingizi mara, Maana Wewe, Bwana, peke yako, Ndiwe unijaliaye kukaa
salama.
Mwanzo
13:17 - Ondoka, ukatembee katika nchi
hii katika mapana yake, na marefu yake, maana nitakupa wewe nchi hiyo.
Mambo
ya Walawi 25:23 - Nayo
nchi haitauzwa kabisa kabisa; kwani nchi ni yangu mimi; maana ninyi ni
wageni na wasafiri wangu.
Kumbukumbu
la Torati 11:24A - Kila
mahali mtakapokanyaga kwa nyayo za miguu yenu patakuwa penu; tokea hilo
jangwa, na Lebanoni, na tokea mto wa Frati, mpaka bahari ya magharibi,
itakuwa ndiyo mipaka yenu.
2
Samweli 22:20 - Akanitoa akanipeleka panapo
nafasi; Aliniponya kwa kuwa alipendezwa nami.
Zaburi
2:8 - Uniombe, nami nitakupa mataifa
kuwa urithi wako, Na miisho ya dunia kuwa milki yako.
Zaburi
107:6, 7 - Wakamlilia Bwana katika dhiki
zao, Akawaponya na shida zao. Akawaongoza kwa njia ya kunyoka, Wapate
kwenda mpaka mji wa kukaa.
Isaya
30:21 - Na masikio yako yatasikia neno
nyuma yako, likisema, Njia ni hii, ifuateni; mgeukapo kwenda mkono wa
kulia, na mgeukapo kwenda mkono wa kushoto.
Waebrania
11:8 - Kwa imani Ibrahimu alipoitwa
aliitika, atoke aende mahali pale atakapopapata kuwa urithi; akatoka
asijue aendako.
Mwanzo
28:15 - Na tazama, mimi nipo pamoja
nawe, nitakulinda kila uendako, nami nitakuleta tena mpaka nchi hii, kwa
maana sitakuacha, hata nitakapokufanyia hayo niliyokuambia.
Kutoka
23:20 - Tazama, mimi namtuma malaika
aende mbele yako, ili akulinde njiani na kukupeleka mpaka mahali pale
nilipokutengezea.
Kutoka
32:34 - Basi sasa uende ukawaongoze
watu hawa mpaka mahali pale ambapo nimekwambia habari zake; tazama,
malaika wangu atakutangulia; pamoja na hayo siku nitakayowajilia
nitawapatiliza kwa ajili ya dhambi yao.
Kutoka
33:14 - Akasema, Uso wangu utakwenda
pamoja nawe, nami nitakupa raha.
Kumbukumbu
la Torati 28:6 - Utabarikiwa uingiapo,
utabarikiwa na utokapo.
Zaburi
105:13-15 - Wakatanga-tanga toka taifa
hata taifa, Toka ufalme mmoja hata kwa watu wengine. Hakumwacha mtu
awaonee, Hata wafalme aliwakemea kwa ajili yao. Akisema, Msiwaguse masihi
wangu, Wala msiwadhuru nabii zangu.
Isaya
59:19B - Basi, wataliogopa jina la Bwana
toka magharibi, na utukufu wake toka maawio ya jua; maana yeye atakuja
kama mkondo wa mto ufurikao, uendeshwao kwa pumzi ya Bwana.
Mathayo
10:1 - Akawaita wanafunzi wake kumi na
wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu, wawatoe, na kupoza magonjwa yote
na udhaifu wa kila aina.
Mathayo
16:19 - Nami nitakupa wewe funguo za
ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa
mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa
mbinguni.
Marko
8:33B - Akageuka, akawatazama
wanafunzi wake, akamkemea Petro, akasema, Nenda nyuma yangu, Shetani;
maana huyawazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu.
Luka
9:1 - Akawaita wale Thenashara,
akawapa uwezo na mamlaka juu ya pepo wote na kuponya maradhi.
Kwa maana ghadhabu ya Mungu imedhihirishwa kutoka
mbinguni juu ya uasi wote na uovu wa wanadamu waipingao kweli kwa uovu.
Kwa kuwa mambo ya Mungu yanayojulikana yamekuwa dhahiri ndani yao, kwa
maana Mungu aliwadhihirishia. Kwa sababu mambo yake yasiyoonekana tangu
kuumbwa ulimwengu yanaonekana, na kufahamika kwa kazi zake; yaani, uweza
wake wa milele na Uungu wake; hata wasiwe na udhuru; kwa sababu,
walipomjua Mungu hawakumtukuza kama ndiye Mungu wala kumshukuru; bali
walipotea katika uzushi wao, na mioyo yao yenye ujinga ikatiwa giza.
Wakijinena kuwa wenye hekima walipumbazika; wakaubadili utukufu wa Mungu
asiye na uharibifu kwa mfano wa sura ya binadamu aliye na uharibifu, na ya
ndege, na ya wanyama, na ya vitambaavyo. Kwa ajili ya hayo Mungu aliwaacha
katika tamaa za mioyo yao, waufuate uchafu, hata wakavunjiana heshima
miili yao. Kwa maana waliibadili kweli ya Mungu kuwa uongo, wakakisujudia
kiumbe na kukiabudu badala ya Muumba anayehimidiwa milele. Amina. Hivyo
Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu, hata wanawake wakabadili
matumizi ya asili kwa matumizi yasiyo ya asili; wanaume nao vivyo hivyo
waliyaacha matumizi ya mke, ya asili, wakawakiana tamaa, wanaume
wakiyatenda yasiyopasa, wakapata nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo
haki yao. Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu
aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa. -Warumi
1:18-28