Thursday, June 30, 2016

KUMTUMIKIA MUNGU

Luka 13:22 - Mtu mmoja akamuuliza Bwana Yesu Je! Watu wanaookolewa ni wachache? Bwana akamjibu akamwambia jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawambia kuwa wengi watataka kuingia wasiweze.
Mahali pengine maandiko yanasema  tangu enzi za Yohana mbatizaji habari njema ya ufalme inahubiriwa, na wenye nguvu wauteka huo ufalme.
KUMTUMIKIA MUNGU
Katika Mathayo 19:27 tunaona maneno ambayo mtume Petro alimuuliza Bwana Yesu kuwa walikuwa wameacha vitu vyote na kumfuata Yesu, Je! Watapata NINI? Mara nyingi napenda kusema kuwa hakuna mtu yeyote duniani mwenye akili timamu anayependa HASARA. Petro alitaka kujua atakachokipata, baada ya kuwa ameamua kuacha vyote na kumfuata Yesu. Kama ingetokea Bwana Yesu amjibu kuwa fanya kazi maana UNAJITOLEA, nadhani hapo ndipo ingekuwa mwisho wa Petro. Lakini kwa kumjibu alimwambia atapata mara mia, katika ulimwengu huu na uzima wa milele baadaye.
Habari hii pia tunaiona katika Marko 10:28-31 huku tofauti ikiwa ni kuongezwa maneno PAMOJA NA DHIKI katika Marko. Ndiyo maana katika Galatia 6:9 mtume Paulo aliandika maneno fulani ili kuwaambia Wakristo waendelee kufanya kazi ya Mungu bila kuchoka, maana malipo yapo baada ya kazi hii katika dunia hii. Maneno hayo ni:
Tena tusichoke katika kutenda mema, kwa maana tutavuna kwa wakati wake tusipozimia roho.
1Kor 15:58; “Basi,ndugu zangu wapendwa, mwimarike, msitikisike, mkazidi sana kutenda kazi ya Bwana siku zote, kwa kuwa mwajua kwamba taabu yenu siyo bure katika Bwana”.  Yaani kazi ambayo italipwa ni ile iliyofanywa katika Bwana,( sio kazi yoyote, katika Bwana. Ndiyo maana anasema ni wale tu wafanyao MAPENZI YA BABA YANGU). Kumbe unaweza ukafanya kazi ya Mungu, lakini yakawa siyo mapenzi ya Mungu.
Katika Ebrania 6:10 tunaona kuwa Mungu si dhalimu hata aisahau kazi ya mtu. Hii ina maana kuwa Mungu hawezi kudhulumu mtu yeyote. Ndio maana imeandikwa “kila mtu atavuna kile alichokipanda”.
Faida ya Kumtumikia Mungu.
Faida utakazozipata kama ukiamua kumtumikia Mungu kwa dhati. Faida hizi ni zile utakazopata ukiwapo hapa hapa duniani. Najua tutalipwa pia na mbinguni, lakini leo naongelea faida za hapa hapa duniani.
-Mithali 11:31 – Mwenye haki atalipwa duniani, na mkosaji pia.
-Mithali 11:25 – Nafsi ya mtu mkarimu itawandishwa. Anyweshaye atanyweshwa mwenyewe. Maana yake ni chochote unachofanya kwa watu, ujue na watu pia watakufanyia. Ukifanya ubaya, ndivyo utafanyiwa; Ukifanya wema ndivyo utafanyiwa.
-Mith 12:14 – Utavuna chochote utakachokipanda.
-Mith 20:7 – Chochote utakachokifanya, kizuri au kibaya, utawaachia watoto wako. Wakati mwingine unaweza kudhani uko salama, kumbe utawaachia watoto wako ama BARAKA, au LAANA.  Ukiangalia kwa makini katika 1Falme 4:24-25 kuna maandiko maneno yanayosema kuwa Sulemani alistarehe pande zote. Swali ni kwa nini alistarehe? Hii ni kwa sababu baba yake alikuwa amepigana vita vya kutosha, alikuwa amesukumia mbali maadui kiasi cha kuwa mbali sana na Ufalme wake Sulemani.
-Mith 13:22 – Huwaachia WANA WA WANA–
Unaona sasa imekwenda kwa  WAJUKUU. Ndiyo maana tunasema  Mungu wa IBRAHIM, ISAKA, na YAKOBO. Leo hii watu wengi wanahangaika kwa sababu ya yale ambayo baba, babu zao walifanya; Wao wanahangaika leo, au wanafurahia leo.
-Luka 7:2-5 -Kuna maneno yanayoonyesha jinsi Wazee walivyomwambia Yesu kumtendea jambo jema mtu ambaye aliwajengea sinagogi. Hivyo kwa kuwa alijenga SINAGOGI basi alistahili kutendewa jambo hilo. Kumbukumbu ni muhimu sana. Leo hii kuna watu wameshapita lakini hakuna kumbukumbu lolote. Walikuwa na mali, walikuwa na uwezo, lakini leo hakuna kumbukumbu lolote kuwa walikuwepo duniani.
-Mith 10:27-Kumcha Bwana kwaongeza siku za mtu. Mpendwa Neno linasema wazi wazi kuwa kama utakuwa ni mcha Mungu miaka yako itaongezwa, mahali pengine inasema AKASHIBA SIKU.
Katika Isaya 54:12-17 tunaona faida tupu kama ukimcha Mungu, sitaikopi hapa, tafadhali tafuta muda uisome uone. Waweza soma pia faida tele katika Isaya 43:2 na uone kuwa hakuna hasara yoyote katika kumcha Mungu.
-Ayub 5:19-27. Ayubu alikuwa ni mzee wa siku nyingi hivyo alijua faida tele za kumtumikia Mungu. Ndiyo maana aliandika namna hiyo hapo, ebu soma uone!
Watu waliomtumikia Mungu na kuona faida zake, ambao habari zao tunazipata katika Biblia. Pata muda usome maandiko kuhusu mifano hii:
-Mdo 9:36-Dorkas.
-Isaya 38:1-Hezekiah.
-Esta 3:12-Mordekai.
-Mdo 10:1-Cornelio.

No comments:

Post a Comment