UTAIINUA MISINGI YA VIZAZI VINGI”. Isaya 58:12
Biblia katika Mithali 1:4 inasema ‘Kuwapa wajinga werevu,
na kijana maarifa na hadhari. Pengine huu ni msatri wa ujumla wenye
lengo la kumsaidia kijana awe mwenye tahadhari, mwangalifu, na ajifunze
kufikiri kibiblia na kuchukua tahadhari kubwa kabla kabla ya kutenda,
naam huku akitumia vema maarifa apatayo kuzishinda changamoto zenye
kumkabili kila siku. Zifuatazo ni baadhi ya mbinu zitakazomsaidia kijana
kuzikabili changamoto mbalimbali;
Kijana atafute kujua nini kusudi la Mungu kumleta duniani.
Wafilipi 2:13 inasema ‘Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi
ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake
jema’. Tambua kwamba kabla hujazaliwa alikujua na akakuwekea kusudi lake
unalopaswa kuliishi, maana umeumbwa ili uyatende mapenzi (kusudi) ya
Mungu hapa duniani. Naam ufahamu wa kusudi la Mungu kwako utakusaidi
kuishi kwa malengo na hivyo kukuepusha na kuifuatisha namna ya dunia
hii.
Katika Warumi 12:2 imeandikwa ‘Wala msiifuatishe namna ya
dunia hii; bali mgeuzwe kwa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya
Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza na ukamilifu’. Kijana mwenye kujua
wajibu wake duniani katika kulitumikia kusudi la Mungu atajizuia na
kujiepusha na makundi mabaya, kuipenda dunia, atatumia vizuri fursa ya
teknolojia kwa utukufu wa Mungu na kuwa na matumizi mazuri ya muda.
Kijana huyu atatumia muda na nguvu zake ipasavyo katika
kufanya kazi zenye kumsaidia kujikimu kimaisha ikiwa ameajiriwa au
amejiajiri, na ambaye anasoma atazingatia masomo kwa sababu anajua
anakokwenda, hivyo hataruhusu mambo ya kipuuzi yaharibu ndoto yake
(Waefeso 5:15-17 na Mhubiri 12:1). Hivyo ni jukumu lako kumuuliza Mungu
ili upate kujua kwa nini upo duniani. Hata hivyo, wokovu, ufahamu wa
kutosha wa neno la Mungu, kuomba kimaswali na vipawa ulivyopewa ni
funguo muhimu za kukusaidia kuelewa kusudi la Mungu kwako.
Kijana ajifunze kuishi kwa imani
Waebrania 10:38 inasema ‘Lakini mwenye haki ataishi kwa
imani; Naye akisi-sita, roho yangu haina furaha naye’. Pia katika 1
Yohana 2:14 imeandikwa ‘Nimewaandikia, ninyi vijana, kwa sababu mna
nguvu, na neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi, mmemshinda yule
mwovu’. Ili aweze kuishi kwa imani ni lazima kijana adumu kuongeza
ufahamu wa neno la Mungu na kulitenda. Kwa kuwa chanzo cha imani ni
kusikia na kusika huja kwa neno la Kristo (Warumi 10:17).
Neno la Mungu likikaa kwa wingi litaumba imani kubwa ndani
yake ambayo itamsaidia kushinda kila changamoto zinazolenga kumuondoa
kwenye imani husika. Maarifa yatokanayo na neno la Kristo yatamjengea
uwezo wa kufanya maamuzi sahihi na kuzikabili changamoto za ujana. Naam
kuishi kwa imani kutamsiaida kijana kudumu kuwa mwaminifu na kudumu
kumpenda Mungu bila kuifuatisha namna ya dunia hii na tamaa zake
(Mitahli 12:1a, 1 Timotheo 4:13 – 16, Ayubu 22:19 na Waefeso 5:6).
Kijana ajifunze kuenenda kwa roho
Kuenenda kwa roho ni wito wa Mungu kwa vijana leo ili
waweze kuzishinda changamoto za ujanani. Biblia katika wagalatia 5:16
inasema ‘Basi nasema enendeni kwa roho, wala hamtatimiza kamwe tamaa za
mwili’. Kuenenda kwa roho ni kumpa nafasi Roho Mtakatifu ya kuongoza
maisha yako sawasawa na mapenzi ya Mungu kwako.
Katika kuenenda kwa roho, siku zote, kijana anapaswa
kutafakari mambo yoyote yaliyo ya kweli, ya haki, safi, yenye kupendeza,
yenye sifa njema na yenye kupendeza (Rejea Wafilipi 4:8 na Warumi
8:5). Ukweli ni kwamba kijana hawezi kuzikwepa kabisa changamoto za
mwili kwa sababu mwili ni sehemu ya maisha na siku zote mwili hutamani
ukipingana na roho (Yohana 3:6 na Wagalatia 5:16). Hivyo ni lazima
kijana ajifunze kuenenda kwa roho ili asizitimize tamaa za mwili.
Kijana ajifunze kuruhusu mapenzi ya Mungu yatime kuhusu mwenzi wa maisha.
Najua vijana wengi sana wamejiwekea vigezo vya wenza ambao
wangependa waje kuishi nao kama wanandoa. Ukweli ni kwamba sehemu kubwa
ya vigezo vyao ni vya kimwili na ni kinyume na mapenzi ya Mungu kwenye
maisha yao. Fahamu kwamba licha ya wewe kuwa na vigezo vya mtu
unayefikiri anafaa kuwa mwenza wako na Mungu naye naye ana vigezo vya
mtu anayejua anayekufaa. Naam suala la nani atakuwa mwenza wako kwa
Mungu ni kipaumbele muhimu sana na ndiyo maana unapaswa kumshirikisha
kwa asilimia zote ili akuongoze kufanya maamuzi sahihi (Mithali 19:14,
Isaya 55:8, Mithali 16:1 na Yeremia 29:11).
Ni muhimu kijana awe makini kuhusu maamuzi anayofanya
katika kitafuta mwenzi wa maisha ili yasije kuharibu kusudi la Mungu juu
yake. Kijana anapaswa kujiepusha na makosa mbalimbali katika kutafuta
mwenza ikiwa ni pamoja na; Kutokumshirikisha Mungu katika kutafuta
mwenzi wa maisha, kufanya maamuzi ya mwenzi wake atakuwa nani ndipo
aanze kuomba, Kuficha dhambi, kuwa na vigezo binafsi visivyo sahihi, na
kufanya maamuzi kabla ya wakati.
Naam kuhusu vijana walioko kwenye ndoa, ni muhimu vijana
hao wakajua kwamba ndoa ni wito wa mapungufu na kwamba hakuna isiyo na
mapungufu, hivyo katika ndoa suala muhimu ni kila mmoja kusimama vema
kwenye nafasi yake na kuchukuliana katika mapungufu yenu huku mkilenga
kutafuta na kutenda makusudi ya Mungu ya kuwaunganisha.
Changamoto ni sehemu ya maisha kwa vijana, na madam tupo
katika dunia hii, hakuna namna kijana atishi bila kuzikabili changamoto
husika, naam jambo muhimu kijana ni kuwa makini na maisha yake akijua
nafasi yake katika ufalme wa Mungu ili adumu kuyatenda mapenzi ya Mungu
katika siku zake. Ni imani yangu kwamba somo hili limekuongezea maarifa
katika kuzikabili na kuzishinda changamoto mbalimbali za ujanani.
Mungu wangu na akubariki na kukusaidia maana ndiye aliyeniambia ‘…utaiinua misingi ya vizazi vingi…’ (Isaya 58:12)
Utukufu na heshima vina wewe Yesu! Wastahili BWANA.
wazazi wake. Baada ya kuzungumza na huyu baba kwa upana
nilikubali na kisha nikapanga muda wa kuonana na mke wake. Tulipoonana
alinieleza kile kilichomuumiza na kumpelekea kuondoka kwa mumewe. Katika
kuzungumza kuna wakati yule mama alisema ‘natamani huyu mwanaume
angekufa kabisa’.
Binafsi nilifikiri amekosea nikamuuliza umesemaje? Akarudia
tena kusema natamani afe naamini nitapata amani zaidi kwa maisha yangu
yaliyosalia. Nilipomuuliza kwa nini unafikiri afe? akajibu yeye si mtu
sahihi aliyepaswa kunioa, kwani walikuja wengi sana, kunichumbia, sijui
kwa nini nilimkubali huyu na ndio maana leo naumia hivi.
Nami nikamwoji je unajua athari ya hayo unayosema? Hujui
kwamba akifa nje ya muda na mapenzi ya Mungu, damu yake itadaiwa
mikononi mwako? Kuwaza hivyo ni kukosea sana, tayari mlishafunga ndoa,
na sasa unapaswa kufikiri namna ya kubadilisha maisha ya ndoa yako kuwa
kwenye hali bora zaidi na si kuendelea kubomoa. Ndipo nikamwambia ‘kama
hutazijua na kuzitumia nafasi ulizopewa na Mungu, kamwe amani haiwezi
kuja kwenye ndoa yako’. Ilichukua miezi yule mama kuelewa na kurejea
kwenye nafasi zake, lakini ashukuriwe Mungu naye alifanyia kazi na sasa
amerudi kwa mumewe wanaendelea vema.
Sikia mwanamke unayesoma ujumbe huu, madaam ulikubali
kuolewa, usimpe ibilisi nafasi kwa kuwaza mabaya juu ya mume wako,
ukihoji, kwa nini nilikubali kuolewa na huyu baba, au kusema najuta
kuolewa na huyu baba, au laiti wangekuwa wanabadilisha wanaume
ningebadilisha haraka wa kwangu nk. Kumbuka kutengemaa kwa ndoa yako ni
kufanikiwa kwa makusudi ya ufalme wa Mungu hapa duniani. Changamoto
mnazozipitia kama wanandoa lengo lake ni kuwatoa kwenye nafasi yenu ya
kufanya kile chenye kuujenga ufalme wa Mungu.
Hivyo haijalishi mume wako kakosea nini, wewe mtwike Mungu
fadhaa zako zote, na uwe tayari kusamehe na kusahau, wala usiawaze
mabaya juu yake, kwa kuwa kadri unavyowaza mabaya ndivyo unavyoiingiza
ndoa yako kwenye uharibifu, ndivyo unavyoyaumba na kuyaita mabaya zaidi
yaje kwenye ndoa.
Nafasi yako ni ya thamani sana kwa mumeo
Katika kusoma kwangu Biblia na kufuatilia sana kuhusu nafasi ambazo Mungu amempa mwanamke, nimegundua kwamba nafasi ya mke kwa mume ni ya muhimu sana. Pengine kwa kiasi fulani inafanana na nafasi ya Kristo kwa kanisa, maana ikiwa katika ulimwengu wa roho mwanamke amepewa kuwa Msaidizi, Mshauri, Mlinzi, Mjenzi na Mleta kibali, je haya si sehemu tu ya majukumu ambayo Yesu anayo kwa kanisa lake kwa ujumla?
Katika kusoma kwangu Biblia na kufuatilia sana kuhusu nafasi ambazo Mungu amempa mwanamke, nimegundua kwamba nafasi ya mke kwa mume ni ya muhimu sana. Pengine kwa kiasi fulani inafanana na nafasi ya Kristo kwa kanisa, maana ikiwa katika ulimwengu wa roho mwanamke amepewa kuwa Msaidizi, Mshauri, Mlinzi, Mjenzi na Mleta kibali, je haya si sehemu tu ya majukumu ambayo Yesu anayo kwa kanisa lake kwa ujumla?
Nafasi ulizopewa na Mungu katika ulimwengu wa roho, ni
ishara kwamba kufanikiwa kwa kusudi la Mungu kupitia ndoa yenu
kunategemea sana namna ambavyo mwanamke anazitumia nafasi zake. Naam
zaidi kukubalika, kustawi na kufanikiwa kila mume wako atendalo
kunategemea pia namna ambavyo wewe (mke) utazitumia nafasi zako. Hivyo
kuchelea kwako kutumia vizuri nafasi zako ni kukwamisha kusudi la Mungu
kwenye ndoa yako, familia yako, jamii yako na taifa lako.
Ukweli ni kwamba ‘Mume wako anakuhitaji sana hata kama
maneno na matendo yake hayaonyeshi kwamba anakuhitaji”. Naam, mumeo
anakuhitaji kuliko unavyofikiri, kadri wewe unavyokaa kwenye nafasi yako
ndivyo unavyosaidia familia yako, kijiji chako, kanisa lako na taifa
lako. Naam mume wako anahitaji sana upendo wako,kumbuka upendo ndio
uliomsukuma Kristo aje afe kwa ajili yetu (Yohana 3:16), ingawa hata leo
wapo watu wasiomwamini, wenye kumtukana lakini yeye bado anawapenda.
Upendo wa Kristo ndani yako ukukumbushe kusimama kwenye nafasi zako kwa
ajili ya mumeo.
Naam bado ningeweza kuandika mambo mengine mengi zaidi,
lakini fahamu jambo hili, laiti mwanamke akisimama na kuzitumia nafasi
zake vema, mabadiliko na uponyaji mkubwa kwenye ndoa yake ni matokeo
halisi ya kutarajia. Nafasi hizi tano zinampa fursa mwanamke ya kuruhusu
mawazo ya Mungu kupitia ndoa yake kutimia na kuzuia mawazo ya Ibilisi
kupitia ndoa yake yasitimie. Naam nafasi ya mwanamke katika ndoa ndiyo
inayoamua uzima au mauti ya ndoa yake, nafasi ndizo zinazoamua
kufanikiwa au kufeli kwa ndoa yake.
Hivyo endapo utayaweka mafundisho haya kuanzia sehemu ya
kwanza kwenye matendo si tu ndoa yako itaponywa, bali, maombi yenu
yatasikilizwa, mume wako atapata kibali mbele za BWANA, naam atakuwa
mume bora katika jamii na kufanikiwa katika kila atendalo. Mahusiano na
mawasiliano mazuri yatakuwa sehemu ya maisha yenu na hivyo kurahisisha
kutekelezwa kwa kusudi la Mungu. Ninapomalizia ujumbe huu muhimu
nakushauri usijitazame kama mwanamke wa kawaida bali jifunze kujitazama
kutoka kwenye nafasi zako kama Msaidizi, Mshauri, Mlinzi, Mjenzi na
Mleta kibali, naam na maisha ya ndoa yako yatabadilika.
Mungu wangu akubariki na kuiponya kabisa ndoa yako, kupitia damu na jina la Yesu, amen.
Utukufu na heshima vina wewe Yesu! Wastahili BWANA wangu
No comments:
Post a Comment