- Msiambiane uongo, kwa kuwa mmevua kabisa utu wa kale, pamoja na matendo yake; - Wakolosai 3:9
- Msimlipe mtu ovu kwa ovu. Angalieni yaliyo mema machoni pa watu wote. - Warumi 12:17
- Tukitangulia kufikiri yaliyo mema, si mbele za Bwana tu, ila na mbele ya wanadamu. - II Wakorintho 8:21
- Mizani ya hadaa ni chukizo kwa Bwana; Bali vipimo vilivyo sawasawa humpendeza. Ukamilifu wao wenye haki utawaongoza Bali ukaidi wao wenye fitina utawaangamiza. - Mithali 11:1,3
- Katika kosa la midomo kuna mtego kwa mbaya; Bali mwenye haki atatoka katika taabu. Atamkaye maneno ya kweli hufunua haki; Bali shahidi wa uongo hutamka hila. - Mithali 12:13,17
- Afichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema. - Mithali 28:13
- Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana,
mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii. -
Yakobo 5:16 - lakini tumekataa mambo ya aibu yaliyositirika, wala hatuenendi kwa hila, wala kulichanganya neno la Mungu na uongo; bali kwa kuidhihirisha iliyo kweli twajionyesha kuwa na haki, dhamiri za watu zikitushuhudia mbele za Mungu. - II Wakorintho 4:2
Friday, October 21, 2016
UAMINIFU
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment