Wednesday, June 4, 2014

BY MWAKASEGE

Tafakari ya 19:
Ikiwa ‘kupenda fedha’ kunaweza kukamfanya mpenda fedha, afarakane na Imani yake, ina maana kupenda fedha kunaweza kupoozesha au kuua kabisa nguvu zake za maombi.
Tunasoma katika 1Timotheo 6:10 ya kuwa: “Shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha, ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani na kujichoma kwa maumivu mengi”.
Jihadhari sana katika hili! Hasa unapokuwa kiongozi, na hata kama siyo kiongozi; na labda una mpango wa kuwa kiongozi baadaye! Ni rahisi sana unapokuwa na moyo wa kupenda fedha, moyo wa kumpenda Mungu unapoa, na hali yako ya kumtegemea Mungu kwa njia ya maombi inapungua, na hata wakati mwingine kupotea kabisa.
Unajikuta Imani na tegemeo lako la kupata majibu ya mahitaji yako, unaweka kwenye fedha na kwa wenye fedha badala ya Mungu!
Imeandikwa katika Mhubiri 10:19 kuwa: “…na fedha huleta jawabu la mambo yote”. Hata kama fedha inakuweza kujibu mahitaji yako, usiache ikaharibu uhusiano wako na Mungu katika maombi.

Mungu awabariki sana!!

1 comment: