Tafakari ya 19:
Ikiwa ‘kupenda fedha’ kunaweza kukamfanya mpenda fedha, afarakane na
Imani yake, ina maana kupenda fedha kunaweza kupoozesha au kuua kabisa
nguvu zake za maombi.
Tunasoma katika 1Timotheo 6:10 ya kuwa: “Shina
moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha, ambayo wengine hali
wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani na kujichoma kwa maumivu mengi”.
Jihadhari sana katika
hili! Hasa unapokuwa kiongozi, na hata kama siyo kiongozi; na labda una
mpango wa kuwa kiongozi baadaye! Ni rahisi sana unapokuwa na moyo wa
kupenda fedha, moyo wa kumpenda Mungu unapoa, na hali yako ya kumtegemea
Mungu kwa njia ya maombi inapungua, na hata wakati mwingine kupotea
kabisa.
Unajikuta Imani na tegemeo lako la kupata majibu ya mahitaji yako, unaweka kwenye fedha na kwa wenye fedha badala ya Mungu!
Imeandikwa katika Mhubiri 10:19 kuwa: “…na fedha huleta jawabu la mambo
yote”. Hata kama fedha inakuweza kujibu mahitaji yako, usiache
ikaharibu uhusiano wako na Mungu katika maombi.
Mungu awabariki sana!!
amina Pasta,Barikiwa
ReplyDelete